2021-06-25 22:29:48
Maumivu na Majibu yake
Dunia yetu imetoka mbali sana. Toka enzi za kina Charles Darwin mpaka leo kina Bill Gates na Elon Musk. Miaka ya kabla ya Darwin kulikuwa na umri wa mawe, tukaja umri wa chuma mpaka kufika mapinduzi ya viwanda na Umri aa Taarifa.
Tumepita huko kote na kufika tulipo leo sababu kubwa ni bindamu kujaribu kupata njia rahisi ya kutatua matatizo yake au kupunguza maumivu.
Nadhani unakumbuka namna binadam aligundua moto ili kuweza kupata joto.
Miaka ya 1950s bado kulikuwa na shida ya mawasiliano duniani. Wazungu wakaja na simu.
Mpaka mwaka 2008 gharama za kupiga simu kwenda nje ya nchi zilikuwa juu sana. 2010 ikaja whatsapp na kurahisisha maisha. Tukaweza pata mawasiliano na ndugu zetu wa mbali.
Swali langu kwako, leo hii wewe unapata maumivu yapi au niseme unaona kuna tatizo gani lipo katika jamii ambalo unadhani kuna namna Teknolojia inaweza rahisisha maisha yako.
Mfano binafsi natamani sana kuona Techies wa Tz wakiwa mahala pamoja kujaribu kutatua matatizo ya Tanzania. Hivyo pamoja na wenzangu tunatafuta namna ya kuwaleta pamoja.
Je, wewe una mtazamo gani juu ya maumivu au matatizo yaliyopo katika jamii? Sio lazima uwe na majibu yake ila kama yapo pia ni sawa.
Iwapo haupo huru kuweka jibu lako hapa group, usisite kunifata DM au katika whatsapp yangu kupitia 0753607400.
Karibu.
138 viewsCharles Venny, 19:29