🔥 Burn Fat Fast. Discover How! 💪

Տchool PVH

Logo of telegram channel schoolpvh1 — Տchool PVH Տ
Logo of telegram channel schoolpvh1 — Տchool PVH
Channel address: @schoolpvh1
Categories: Education
Language: English
Subscribers: 11.31K
Description from channel

The center of academic resources
📚 Primary School to teachers college
Android
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.schoolpvh
iOS
https://apps.apple.com/tz/app/school-pvh/id6445867210
📞
255747272228
255626272229

Ratings & Reviews

4.00

2 reviews

Reviews can be left only by registered users. All reviews are moderated by admins.

5 stars

1

4 stars

0

3 stars

1

2 stars

0

1 stars

0


The latest Messages 16

2022-08-24 11:55:49 SENSA YA WATU NA MAKAAZI 2022
MASWALI YATAKAYOULIZWA WAKUU WA KAYA

SEHEMU A: UTAMBULISHO
A01. Tafadhali nitajie idadi ya watu wote waliolala katika kaya hii usiku wa kuamkia siku ya Sensa (23 Agosti 2022)

SEHEMU B: TAARIFA ZA KIDEMOGRAFIA
B01. Orodha ya majina ya wanakaya
B02. Tafadhali nitajie majina ya watu wote waliolala katika kaya hii usiku wa kuamkia siku ya Sensa,
yaani usiku wa Jumatatu kuamkia Jumanne ya tarehe 23 Agosti, 2022, ukianzia na jina la Mkuu wa Kaya.
B03. Je, una uhusiano gani na Mkuu wa Kaya?
B04. Je, ni mwanamme au mwanamke?
B05. Je, una umri wa miaka mingapi?
B06. Je, ni ipi hali ya ndoa kwa hivi sasa?
B07. Tafadhali nitajie namba ya simu ya mkononi

SEHEMU C: TAARIFA YA HALI YA ULEMAVU-WATU WOTE
C01. Je, una ualbino?
C02. Je, una matatizo ya kuona hata ukiwa umevaa miwani?
C03. Je, una matatizo ya kusikia hata kama unatumia shimesikio?
C04. Je, una matatizo ya kutembea au kupanda ngazi?
C05. Je, una matatizo ya kukumbuka au kufanya kitu kwa umakini?
C06. Je, una matatizo ya kujihudumia kama vile kuoga au kuvaa nguo?
C07. Kwa Kutumia Lugha ya Kawaida: Je, una matatizo ya Kuwasiliana kwa kutumia lugha ya kawaida? kwa mfano kuelewa au kueleweka?
C08. Je, una aina nyingine ya ulemavu kati ya hizi zifuatazo?
C09. Je, ni nini chanzo cha ulemavu ulionao?
C10. Je, una kifaa cha usaidizi kwa tatizo/ulemavu ulionao?

SEHEMU D: TAARIFA ZA UHAMAJI
D01. Je, ni raia wa nchi gani?
D02. Je, ni raia wa nchi zipi?
D03. Kwa kawaida unaishi Mkoa/Nchi gani?
D04. Je, kwa kawaida huwa unashinda wapi?
D05. Je, ulizaliwa Mkoa/Nchi gani?
D06. Je, ulikuja lini kuishi katika mkoa huu/nchini Tanzania?
D07. Je, umeishi kwa muda gani katika mkoa huu/Nchini Tanzania?
D08. Je, ulikuwa unaishi wapi kabla ya kuhamia hapa?
D09. Je, ni ipi sababu kuu ya kuhamia mkoa huu/nchini Tanzania?
D10. Je, ulikuwa unaishi Mkoa/Nchi gani wakati wa Sensa ya mwaka 2012?
D11. Je, ulikuwa unaishi Mkoa/Nchi gani mwaka 2021?

SEHEMU E: TAARIFA ZA VITAMBULISHO VYA UTAIFA NA UHAI WA WAZAZI
E01. Je, una vitambulisho vifuatavyo?
A. Je, una nyaraka zifuatazo za kitaifa?
B. Je, una kitambulisho cha mjasiriamali?
C. Je, baba mzazi wa yuko hai?, Je mama mzazi wa yuko hai?

SEHEMU F: TAARIFA ZA ELIMU: WATU WENYE UMRI WA MIAKA 4 AU ZAIDI
F01. Je, unajua kusoma na kuandika katika lugha ya Kiswahili, Kiingereza, Kiswahili na Kiingereza
au lugha nyingine yoyote?
F01A. Je, unaweza kufanya hesabu rahisi za kujumlisha, kutoa, kugawanya na kuzidisha katika
shughuli zako za kila siku?
F02. Je, kwa hivi sasa unasoma, uliachia, umemaliza au hujawahi kwenda shule/skuli?
F03. Je, ni ipi ilikuwa sababu kuu ya kuacha/kutowahi kwenda shule/skuli?
F04. Je, ni kiwango gani cha elimu ulichomaliza au uliachia au unachosoma kwa sasa?

SEHEMU G: TAARIFA ZA SHUGHULI ZA KIUCHUMI: WATU WENYE UMRI WA MIAKA 5
AU ZAIDI
G01. Katika kipindi cha wiki moja iliyopita, Je, ni kazi/shughuli gani kati ya zifuatazo ulitumia muda
mwingi zaidi kuifanya?
G02. Ingawa hukufanya shughuli yoyote wiki iliyopita, Je, unayo kazi ya kuajiriwa, shughuli katika
shamba lako au katika biashara yako ambayo hukufanya wiki iliyopita na unatarajia kuendelea
nayo?
G03. Je, umefanya jitihada yoyote ya kutafuta kazi au shughuli katika kipindi cha wiki nne (4)
zilizopita?
G04. Je, Kwa sasa uko tayari kuanza kazi ya malipo au aina yoyote ya biashara, kilimo au kazi yoyote
kama nafasi ikitokea?
G05. Katika shughuli kuu, Je, ulikuwa huwa unajishughulisha na nini?
G06. Je, shughuli kuu unayofanya inamilikiwa na nani?
G07. Je, ni ipi shughuli kuu ya kiuchumi katika biashara au mahali unapofanyia kazi?
G08. Je, katika kipindi cha miezi 12 iliyopita yaani kuanzia Agosti 2021 mpaka usiku wa kuamkia
siku ya Sensa, ulifanya kazi kama mchimbaji mdogo wa mchanga au madini yafuatayo?
1.5K views08:55
Open / Comment
2022-08-23 22:05:40 SchoolPvh Application A Standard Online Education Learning Platform
Primary School 1-7
Secondary School 1-6
Teachers College GATC & DSE

Install through the link
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.schoolpvh

SchoolPvh App have the following content
Lesson Notes
Practicals Notes
Necta Solved past papers
All syllabus
Reference Books
All exams Package
FOR
Primary School 1-7
Secondary School 1-6
Teachers College GATC & DSE

Install through the link
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.schoolpvh

OR Visit schoolpvh website
www.schoolpvh.ac.tz

Exams package For Telegram User
https://t.me/pvh_exams
1.8K views19:05
Open / Comment
2022-08-23 09:51:28
2.0K views06:51
Open / Comment
2022-08-16 21:56:19
Idadi kubwa ya Wahitimu hukosa ajira kwasababu fani walizosoma ni tofauti na mahitaji
Je unakubaliana na Hoja hii?
4.0K views18:56
Open / Comment
2022-08-15 09:06:39 FORM FIVE THIRD SELECTION
Angalia wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha tano 2022/2023 awamu ya tatu
@schoolpvh1
http://selform.tamisemi.go.tz/Content/selection-and-allocation/2022/third-selection/index.html
4.4K viewsedited  06:06
Open / Comment
2022-08-11 20:44:57 Halafu kesho tutaelezeana humu humu kwa comments je tunajionaje baada ya miaka 3/4 ya chuo.
Mwisho kabisa, kumekuwa na wanafunzi wengi waliomaliza michepuo mbalimbali wakiomba ushauri juu ya nini cha kusomea chuo kikuu na ambapo akimaliza ataajiriwa,nawaomba sana tuwaambie wakasome vitu wavipendayo na sio vitu vitakavyowapa ajira ya kuajiriwa wakimaliza masomo yao mfano,Kuna mwalimu wa wito na mwalimu alietaka sehemu ya kuajiriwa tu.

Nawasilisha.
@schoolpvh1
Imeandaliwa na #Khadija Mtalame
5.4K views17:44
Open / Comment
2022-08-11 20:44:57 Ushauri kwa waliomaliza Kidato cha 6 (baada ya matokeo): Nini cha kusomea Chuo Kikuu Kupambana na Soko la Ajira


Mambo yafuatayo yanapaswa kuzingatiwa katika kuelekea kuchagua masomo ya chuo kikuu,

MOJA,

Vijana wote wanaotaka kufanya maombi ya chuo kikuu wanatakiwa kuhakikisha kwamba WANAISHI NDOTO ZAO, kutokana na kuwepo kwa shida ya ajira ambapo kumekuwa na wahitimu wengi ambao wameshindwa kujiajiri na kuajirika kutokana na namna elimu walivyopata.

Mwanafunzi au mtu yoyote anaetaka kufanya chaguzi ya fani ya kusomea chuo kikuu anatakiwa kwanza kujipima na kuangalia Nini anapenda maishani mwake? Na sio akasomee kitu gani chenye ajira. Mfano, unaweza kukuta kipaumbele Cha serikali ya JMT Ni afya na ualimu sayansi na ukaamua kwenda kusoma katika kada hizo,lakini mwisho wa siku ukamaliza na ukasubiriwa kuajiriwa na endapo hutaajiriwa elimu yako itapotea pia utakuwa umepoteza ndoto zako.

Lakini, endapo mtu ukaamua kusoma kitu unachokipenda moyoni mfano, endapo unapenda kuwa fundi mshonaji wa nguo tangu ukiwa mdogo,Ni lazima uhakikishe kwamba unachagua masomo ambayo ukienda kusoma darasani utakuwa na amani ya moyo na utayapenda sana ,ambapo mwisho wa siku utaelewa na hautakuwa mzigo mtaani Mara utakapomaliza masomo yako.

Hivyo,nawashauri sana vijana muombe vitu ambavyo mnavipenda kutoka moyoni na sio vitu ambayo unahisi au umeshauriwa vina ajira endapo utamaliza,siku hizi hakuna kitu utasoma kitakupa ajira moja kwa moja, hata aliesomea Udaktari anaweza kumaliza na asiajiriwe lakini endapo utasoma Udaktari kwa kupenda hata usipoajiriwa utaweza kujiajiri mwenyewe.

Hivyo napenda kuwaasa, vijana na watanzania wote kwamba ILI TUWEZE KUPAMBANA NA AJIRA KWA WAHITIMU WA VYUO VIKUU,tafadhali tuhakikishe kwamba tuwaambie vijana wetu wakasome vitu wanavyovipenda na sio kitu ambacho anahisi ataweza kuajiriwa endapo akimaliza masomo yake.

PILI, ni ndoto ya kila mwanafunzi anaposoma anakuwa amedhamiria kuwa nani na kwasababu gani. Kwa kuzingatia hilo nipende kuwaambia vijana waliomaliza kidato Cha sita elimu ya chuo kikuu siyo "fashion" kwamba ilimradi nimesoma elimu ya chuo kikuu, jipe nafasi jitafakari angalia mbele miaka 3/4/5 ijayo unataka kuwa nani, hakuna kinachoshindikana, kuamua, kudhamiria na kuchukua maamuzi ni sehemu muhimu katika maisha yenu yote hivyo basi ni vyema kuwa makini zaidi katika wakati wote ambao unajitizama baada ya miaka 3/4 ya kumaliza chuo utakuwa wapi na unafanya nini!

Usikubali kubaki ulipo, usikubali kurudishwa nyuma na marafiki ulionao, amka simama imara chagua kitu kitakachokufanya baada ya miaka 3/4 ya chuo kikuu unakuwa kweli watofauti kubwa.
Ni kweli ajira hakuna hasa zinazotoka serikalini kwa maana ni chache na zina ushindani mkubwa, kama lengo lako hasa ni ukimaliza upate ajira serikalini basi utakuwa hujaamua kuwa nani baada ya miaka ya chuo.

Tuwe na tabia ya kujitizama na kujiwekea malengo makubwa lakini yanayofikika katika maisha yetu ya Chuoni na yakila siku, kwa kuzingatia hili tuwe tayari kuweka mawasiliano sahihi na watu sahihi kwa muda sahihi, tujitahidi kutafakari pale unarudi nyumbani baada ya miaka ya chuo na upo upo tu unaangalia wazazi, tukumbuke suala la kujituma kwa moyo wa dhati liwe kipaumbele chetu kikubwa.

Kumbuka; nyakati zinabadilika Ila mtazamo wa wewe uwe nani baada ya miaka ya chuo unao wewe na wewe ndo kiongozi mkubwa.

Usiende chuo kikuu kwasababu nimechaguliwa kwenda lazima niende, hapa naelezea kidogo jambo, elimu ya chuo kikuu siyo fashion kwamba baada ya miaka 3 ukiona ulichosoma hakifai utarudi tena ukasome kingine, mafanikio yako unayo wewe fanya maamuzi sahihi leo ili kesho ukawe mshindi katika jamii yako na familia yako. Acha kufuata mkumbo.

Leo nakupa kazi ya kufanya kijana uliyechaguliwa kwenda chuo kikuu, tenga saa moja kaa pahala patulivu kuwa na notebook yako na kalamu, zima simu yako, sali kwa imani yako kisha anza kuandika unataka nini baada ya miaka 3 /4 ya chuo kikuu kisha tafakari je ninachoomba kitanifikisha hapo?
4.9K views17:44
Open / Comment
2022-08-11 10:46:10
Ni uongo upi aliutumia mwanafunzi wako!
Ukaja gundua kakudanganya badae
3.8K views07:46
Open / Comment
2022-08-11 08:44:44
Tanzania......!
3.8K views05:44
Open / Comment
2022-08-06 17:55:56 WITO WATOLEWA MATUMIZI YA LUGHA YA KUFUNDISHIA, UBORESHAJI SERA YA ELIMU


@schoolpvh1

Wito umetolewa wa kufanya matayarisho ya kutosha ya matumizi ya lugha itakayokubalika kufundishia hasa kwa upande wa walimu na wanafunzi katika ngazi zote za Elimu nchini.

Wito huo umetolewa na Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Mwanahamisi Ameir wakati akifungua kikaokazi cha maoni ya uchambuzi na tathmini ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014 kinachofanyika Zanzibar.

Amesema kuwa matayarisho ya walimu upande wa mafunzo ni ya muhimu katika kuhakikisha walimu wapya wanaozalishwa na ambao wapo tayari kazini wanakuwa na vigezo vinavyotakiwa.

"Matayarisho ni ya muhimu kujua vitu kama sifa za wanaoenda kusomea ualimu, sifa za vyuo, muda wa mafunzo uweje, matayarisho ya walimu kumudu lugha husika ya kufundishia, vyote hivi vitolewe kwa kiwango katika vyuo vyote ili kupata walimu wenye sifa stahiki," amefafanua Ameir.

Akiongea katika kikao hicho, Mwenyekiti wa timu ya Mapitio ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014, Prof. Joseph Semboja amesema lengo la kikaokazi hicho ni kupokea maoni kutoka kwa wadau wa elimu kutoka upande wa Zanzibar juu ya maboresho ya Sera hiyo.

@schoolpvh1
5.2K viewsedited  14:55
Open / Comment