Get Mystery Box with random crypto!

Տchool PVH

Logo of telegram channel schoolpvh1 — Տchool PVH Տ
Logo of telegram channel schoolpvh1 — Տchool PVH
Channel address: @schoolpvh1
Categories: Education
Language: English
Subscribers: 11.31K
Description from channel

The center of academic resources
📚 Primary School to teachers college
Android
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.schoolpvh
iOS
https://apps.apple.com/tz/app/school-pvh/id6445867210
📞
255747272228
255626272229

Ratings & Reviews

4.00

2 reviews

Reviews can be left only by registered users. All reviews are moderated by admins.

5 stars

1

4 stars

0

3 stars

1

2 stars

0

1 stars

0


The latest Messages 31

2022-04-16 13:21:45 DIRISHA LA KUTUMA MAOMBI KADA YA AFYA LAFUNGULIWA

Sifa za Mwombaji
Awe raia wa Tanzania
Awe na umri usiopungua miaka 18 na usiozidi Umri wa miaka 45
Awe hajawahi kuajiriwa Serikalini na kupata cheki namba na endapo mwombaji atakuwa alishaajiriwa Serikalini na kupata Cheki Namba, atatakiwa kuzingatia Utaratibu wa uhamisho au kurejea katika Utumishi wa Umma baada ya kuacha kazi kama ilivyobainishwa kwenye Waraka Na. CCB.228/271/01 wa tarehe 07 Agosti, 2012.
Mwombaji awe na sifa na weledi kwa Mujibu wa Waraka wa Maendeleo ya Utumishi Namba. 1 wa mwaka 2009 kuhusu kada zilizo chini ya Wizara ya Afya kama zilivyoainishwa hapo juu.
@schoolpvh1
             
Maombi yote yaambatishwe na nyaraka zifuatazo
Nakala ya cheti cha kuzaliwa
Nakala ya cheti cha Kidato cha Nne/Sita
Nakala ya Vyeti vya Taaluma (Cheti na Transcripts)
Nakala ya cheti cha Usajili Kamili (Full Registration)
Waombaji waliosoma nje ya Nchi waambatanishe na Ithibati (Accreditation) kutoka Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU).
Cheti cha Mafunzo kwa Vitendo (Internship)
Maelezo Binafsi (CV)
Picha ndogo (passport size) ya hivi karibuni
@schoolpvh1
           

Maelezo ya ziada kuzingatia

Waombaji watakaochaguliwa watapangiwa kazi kwenye maeneo yenye upungufu mkubwa wa watumishi. Hivyo utatakiwa kuchagua eneo ambalo ungependa kupangiwa endapo utafanikiwa kupata nafasi hiyo; Aidha, hakutakuwa na kubadilisha kituo pindi utakapopata nafasi hiyo

Nakala za Vyeti vyote vithibitishwe na Mahakama au Wakili

Waombaji wanaojitolea katika mikoa mbalimbali waambatishe barua inayomtambulisha kutoka kwa Mganga Mkuu/Mfawidhi wa Mamlaka husika.

Maombi yote yatumwe kwa njia ya mtandao (online) kupitia mfumo wa kielektroniki unaopatikana kupitia anuani ifuatayo ajira.moh.go.tz

Maombi yoyote yatakayowasilishwa kwa njia ya posta au kuletwa moja kwa moja ofisini hayatafanyiwa kazi.

Mwisho wa kupokea maombi ni tarehe 29 April, 2022 saa 9.30 Alasiri.

Kwa maelezo zaidi jinsi ya kutumia mfumo huu pakua maelezo haya
@schoolpvh1
1.8K viewsedited  10:21
Open / Comment
2022-04-14 21:25:23 Matokeo ya Usahihishaji wa Rufaa za Watahiniwa wa Mtihani wa
KIDATO CHA NNE (CSEE) NOVEMBA 2021 - AWAMU YA I
2.3K viewsedited  18:25
Open / Comment
2022-04-14 21:22:15 Matokeo ya Usahihishaji wa Rufaa za Watahiniwa wa UpimajiMtihani wa
KIDATO CHA PILI (FTNA) NOVEMBA 2021 - AWAMU YA I
2.3K viewsedited  18:22
Open / Comment
2022-04-14 21:02:10 NAMNA YA KUMSAIDIA MTOTO KUWA MTU BORA KWENYE JAMII

1. Mfundishe kufanya kazi kwa Ushirikiano (Teamwork). Mfano unaweza kutenga muda kusaidiana naye kwenye kufanya 'Homework' au majukumu madogo madogo ya Nyumbani akishirikiana na Wenzake

2. Shiriki au Mfundishe kupanga malengo pamoja na maono mliyonayo. Hili linaweza kuwa gumu kwasababu Wazazi wengi wana asili ya kuamua kila kitu wanachoamini ni kizuri kwaajili ya Watoto wao

3. Washirikishe Watoto kwenye uwekaji wa Sheria/Miongozo itakayowasaidia wawe na tabia njema. Mtoto wako anapohusika na kuwajibika kwenye uwekaji wa sheria zilizo katika familia, atakuwa na uwezekano mkubwa wa kuzifuata.

@schoolpvh1
2.4K views18:02
Open / Comment
2022-04-14 17:20:44 TAMISEMI YAOMBA KIBALI CHA KUAJIRI WALIMU WAPYA ELFU 10


Waziri wa TAMISEMI, Innocent Bashungwa leo amewasilisha Bungeni makadirio ya mapato na matumizi ya mwaka wa fedha 2022/2023 ambapo amesema TAMISEMI imeomba kibali cha kuajiri Walimu wapya Elfu 10.

"Takwimu zilizopo zinaonesha kuwa kuna Shule za Msingi 17,034 zenye Wanafunzi 12,033,594 wakiwemo wenye mahitaji maalum 60,825 na Shule za Sekondari 4,175 zenye Wanafunzi 2,607,142 wakiwemo wenye mahitaji maalum 11,106, jumla ya Walimu waliopo ni 258,291 wakiwemo wa Shule za Msingi 173,591 na Sekondari Walimu 84,700"

"Hadi Machi, 2022 mahitaji ya Walimu Shule za Msingi ni 274,549 kwa uwiano wa 1:60 (Mwalimu mmoja kwa Wanafunzu 60), waliopo ni 173,591 na upungufu ni 100,958 sawa na 36.77% ya mahitaji, mahitaji ya Walimu kwa Wanafunzi wenye mahitaji maalum kwa Shule za Msingi ni 3,631, waliopo ni 1,517 na upungufu ni Walimu 2,143 sawa na 59.02% ya mahitaji, mahitaji ya Walimu kwa Shule za Sekondari ni 159,443 waliopo ni 84,700 na upungufu ni 74,743 sawa na 46.87%"

"Katika kukabiliana na upungufu wa walimu uliopo, TAMISEMI imeomba kibali cha kuajiri Walimu 10,000 wa Shule za Msingi na Sekondari, kati ya hao 5,000 ni kwa ajili ya Shule za Awali na Msingi na 5,000 kwa ajili ya Shule za Sekondari, hii itapunguza mahitaji ya Walimu wa Shule za Sekondari kwa asilimia 6.56 na elimu ya Awali na Msingi kwa asilimia 10.65"

@schoolpvh1
2.4K viewsedited  14:20
Open / Comment
2022-04-13 07:58:45 NAFASI ZA AJIRA 9800 ZA WALIMU 2022 ZATANGAZWA
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Jenista Mhagama amesema ajira mpya 32,604 zinazotarajiwa kutangazwa kabla ya kufikia mwisho wa mwaka huu wa fedha, zitaigharimu serikali Sh bilioni 315 kwa mwaka.

Mhagama ametoa kauli hiyo leo Aprili 12, 2022 jijini Dodoma akizungumza kuhusu utoaji wa vibali vya ajira kwa watumishi wa umma nchini.

Amesema kati ya ajira hizo 32,604, sekta zilizopewa kipaumbele ni elimu iliyopewa nafasi12,035, afya 10,285 na sekta zingine nafasi 2,392.

Amesema katika nafasi 12,035 za sekta ya elimu, nafasi 9,800 ni kwa wa walimu wa shule za msingi na sekondari, ambapo mchakato wake utasimamiwa na TAMISEMI, ilihali nafasi 2,235 ni kwa ajili ya wahadhiri wa vyuo vikuu, vyuo vya elimu ya juu na wakufunzi wa vyuo vilivyopo chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, ambapo mchakato utasimamiwa na taasisi husika kwa kushirikiana na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.

Kwa upande wa sekta ya afya, Mhagama amesema imekasimiwa nafasi za ajira 10,285 zinazojumuisha nafasi 7,612 kwa ajili ya hospitali, vituo vya afya na zahanati zilizopo katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, ambapo mchakato utasimamiwa na TAMISEMI.

Amesema nafasi 1,650 kwa ajili ya watumishi wa kada za afya katika Hospitali za Kanda, Hospitali za Rufaa za Mikoa ambapo mchakato wake utasimamiwa na Wizara ya Afya.

Pia amezitaja nafasi 1,023 kwa ajili ya vyuo vya afya, hospitali nyingine za kimkakati na zile za Mashirika ya Dini na hiari zenye mkataba na serikali.

Mhagama pia amefafanua nafasi 2,392 zinazotarajiwa kujazwa kwenye sekta zingine za kipaumbele kuwa katika kada za kilimo nafasi za ajira ni 814, kada za mifugo nafasi 700, kada za uvuvi nafasi 204, kada za maji nafasi 261 na kada za sheria nafasi 513.

Amesema mchakato wa ajira hizo utasimamiwa na wizara husika pamoja na Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.

Waziri amefafanunua kuwa zipo nafasi 7,792 kwa ajili ya watumishi wa kada nyingine kwenye wizara, idara zinazojitegemea, Wakala wa Serikali, Mamlaka za Serikali za Mitaa na taasisi nyingine za umma.
@schoolpvh1
3.2K viewsedited  04:58
Open / Comment
2022-04-12 21:55:19 2022 NECTA TIMETABLE
SFNA
PSLE
ACSEE
DSEE
GATCE
GATSCCE

Download Kupitia link hii
https://www.schoolpvh.ac.tz/2022/02/necta-2022-timetables.html?m=1
3.8K views18:55
Open / Comment
2022-04-12 21:33:19 TAARIFA YA WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA
UMMA NA UTAWALA BORA, MHE. JENISTA JOAKIM MHAGAMA (MB.) KWA
WAANDISHI WA HABARI KUHUSU UTEKELEZAJI WA AHADI YA SERIKALI YA
KUAJIRI WATUMISHI WAPYA 44,096, KUPANDISHA VYEO WATUMISHI 92,619 NA
KUBADILISHA KADA WATUMISHI 6,026 KWA MWAKA WA FEDHA 2021/2022
2.9K viewsedited  18:33
Open / Comment